Gör Mahia ni klabu ya kandanda yenye makao yake katika mji mkuu wa Nairobi nchini Kenya. Ni mmojawapo wa vilabu viwili maarufu zaidi nchini katika kandanda ya vilabu nchini Kenya (klabu nyingine maarufu na mpinzani wake wa jadi ni AFC Leopards). Gör Mahia imeshinda Ligi ya Kenya mara 11 na Kombe la Kenya mara nane. Gör Mahia ndiyo klabu ya kipekee nchini Kenya kushinda Taji la bara Afrika, kwani klabu hii ilishinda Kombe la Afrika la mabingwa mwaka wa 1987. Klabu hii ilianzishwa mwaka wa 1968 wakati vilabu viwili vya kandanda,Luo United na Luo Sports Club (pia ilikuwa inajulikana kama Luo Stars) , viliungana. Mmoja wa mwanzilishi wake alikuwa mwanasiasa Tom Mboya. Uwanja wao wa kucheza mechi za nyumbani ni Nairobi City Stadium.
Je,uwanja wa nyumbani ya klabu ya Gor Mahia ni gani?
Ground Truth Answers: Nairobi CityNairobi City StadiumNairobi City Stadium
Prediction: